MSANII wa filamu Bongo, Jimmy Mafufu amewabwatukia mastaa wenye tabia za  chuki za kuwaroga wenzao na kuwarudisha nyuma kimaendeleo.
Jimmy Mafufu.
Akichonga na paparazi wetu, Mafufu alisema anashangazwa jinsi wasanii wasivyopenda mafanikio ya wengine wakati usanii hauna uhusiano wowote na chuki, fitna na majungu.
“Hii ni roho mbaya na ya kishetani, yaani wasanii wengi wamejiingiza kwenye vitendo vya kishirikina ili kuwaumiza wengine, tasnia imejaa majungu, wasisahau Mungu yupo na anaona,” alisema Mafufu.

0 comments:

Post a Comment

 
Top
Blogger Template